Mwaka 1971, Chama Cha Mapinduzi kilianzisha rasmi Sera ya Chama Kushika Hatamu. Kwa mujibu wa sera hii, Chama ndicho kilikuwa na nguvu, mamlaka na madaraka kuliko chombo kingine chochote nchini. Katika kutekeleza sera hiyo, Kivukoni College kililazimika kufanya mageuzi bila ya mabadiliko ya kisheria.
Jina la Chuo lilibadilika na kuwa Chuo cha Chama Kivukoni (Kivukoni Ideological College).
Jukumu kuu la Chuo lilikuwa kufundisha Itikadi ya Chama ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea kwa viongozi wa Chama, Serikali na Mashirika ya Umma, Kufanya Utafiti na kutoa ushauri kwa Chama.
No comments:
Post a Comment