Nchi yetu ilirejea rasmi kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa kuanzia tarehe 1 Julai, 1992.
Chuo cha Chama Kivukoni kililazimika kufanya mageuzi ambayo yangeendana na mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Chuo zilikuwa zifuatazo:- 3 50th Anniversary
(1) Kusajili upya Chuo chini ya Sheria ya Makampuni (Sura 212) tarehe 20 Novemba, 1992.
(2) Chuo kilitambulika rasmi kwa jina la Chuo cha Sayansi Jamii Kivukoni (Kivukoni Academy of Social Sciences).
(3) Vyuo vyote vya Kanda, isipokuwa Chuo cha Kanda cha Zanzibar, vilifungwa. Chuo cha Lushoto kiliuzwa kwa Idara ya Mahakama, Chuo cha Kihinga kiliuzwa kwa Kanisa Katoliki, Jimbo la Kigoma na Vyuo vingine vitano vilivyobaki vilikabidhiwa Serikalini.
(4) Majukumu makuu ya Chuo yalibadilika. Chuo kilikuwa na majukumu yafuatayo:-
(a) Kufundisha taaluma katika Sayansi Jamii, hususan programu za mafunzo zifuatazo:-
• Stashahada katika Sayansi Jamii (Diploma in Social Sciences)
• Stashahada katika Maendeleo ya Uchumi (Diploma in Economic Development)
• Stashahada ya Masuala ya Jinsia katika Maendeleo (Diploma in Gender Issues in Development)
• Cheti katika Kazi za Vijana (Certificate in Youth Work).
(b) Kufanya tafiti katika masuala ya Sayansi Jamii na
(c) Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa sekta ya umma na sekta binafsi. 4 50th Anniversary
No comments:
Post a Comment